Mwenyezi Mungu alisema,Kazi ambayo Yehova Alifanya kwa Waisraeli ilianzishwa miongoni mwa ubinadamu, chanzo cha mahali rasmi pa Mungu hapa ulimwenguni, pahali patakatifu ambapo Alikuwepo. Hii kazi Aliiwekea mipaka miongoni mwa watu wa Israeli tu. Kwanza, hakufanya kazi nje ya Israeli; badala yake, Alichagua watu Alioona kwamba walifaa ili kuwawekea mipaka upana wa kazi Yake.
Israeli ndipo mahali ambapo Mungu Aliwaumba Adamu na Hawa, na kutoka kwenye vumbi la mahali hapo, Yehova Alimwumba mwanadamu; ndio msingi wa kazi Yake ya hapo ulimwenguni. Waisraeli, ambao ni kizazi cha Nuhu na Adamu, ndio waliokuwa msingi wa kazi ya Yehova ulimwenguni.
Umuhimu, kusudio, na hatua ya kazi ya Yehova nchini Israeli vyote vilikuwa vya kuanzisha kazi Yake katika ulimwengu mzima, na taratibu kuieneza kwenye mataifa mengine kutoka kwenye kitovu chake cha Israeli. Hii ndiyo kanuni ambayo Alitumia katika kufanya kazi kotekote ulimwenguni—kuanzisha mfano, kisha kuupanua mpaka watu wote ulimwenguni waweze kukubali injili Yake. Waisraeli wa kwanza walikuwa kizazi cha Nuhu. Watu hao walikuwa tu na pumzi za Yehova, na waliweza kujitunza wakatilia maanani mahitaji ya kimsingi ya maisha, lakini hawakujua Yehova Alikuwa Mungu aina gani, wala hawakujua mapenzi Yake kwa binadamu, na hata namna ambavyo walitakikana kumstahi Bwana wa viumbe vyote. Vizazi vya Adamu havikujua ni taratibu na sheria gani ambazo lazima wangetii, au ni kazi gani ambayo viumbe lazima wafanyie Muumba. Kile walichojuatu kilikuwa kwamba mume lazima atoke jasho na atie bidii ili kutosheleza familia yake, na kwamba mke lazima amtii mume wake na kuendeleza kizazi cha binadamu ambacho Yehova Aliumba. Kwa maneno mengine, watu hawa walikuwa tu na pumzi za Yehova na maisha Yake, lakini hawakujua namna ya kufuata sheria za Mungu au namna ya kutosheleza Bwana wa viumbe vyote. Walielewa kidogo sana. Kwa hivyo ingawaje hakukuweko na chochote kisichostahili au chenye ujanja katika mioyo yao, na ingawaje ilikuwa nadra sana kwao kuwa na wivu au hata ugomvi, hawakujua wala kuelewa Yehova, Bwana wa viumbe vyote. Vizazi hivi vya binadamu vilijua tu kula kile ambacho Yehova Alikuwa Ameunda, kufurahia kile ambacho Yehova Alikuwa ameunda, lakini hawakujua kustahi Yehova; hakiwajua kile ambacho kilistahili kufanywa ili kumwabudu Yeye huku wakiwa wamepiga magoti. Wangeitwaje viumbe Vyake? Na kwa hiyo, haya maneno “Yehova ni Bwana wa viumbe vyote” na “Alimwumba binadamu kama dhihirisho Lake yeye mwenyewe, kujitukuza na kumwakilisha,” hayakusemwa bure bilashi? Watu wasiomstahi Yehova wanawezaje kuwa agano katika utukufu Wake? Wanawezaje kuwa dhihirisho la utukufu Wake? Haya maneno ya Yehova “Nilimwumba binadamu kwa mfano Wangu” yakawa silaha kwenye mikono ya Shetani—yule mwovu? Je, haya Maneno hayawi ya alama ya udhalilishaji kwa uumbaji wa binadamu na Yehova? Ili kukamilisha awamu hiyo ya kazi, Yehova, baada ya kumwumba mwanadamu, hakumwelekeza wala kumwongoza kuanzia kwa Adamu hadi Nuhu. Haukuwa mpaka wakati wa mafuriko ndipo Alianza rasmi kuwaongoza Waisraeli waliokuwa vizazi vya Adamu na Nuhu. Kazi na maneno Yake nchini Israeli vyote viliongoza maisha ya watu wote kotekote nchini, vikiwaonyesha kwamba Yehova hakuweza tu kutia pumzi kwenye binadamu, ili apate maisha yake, na afufuliwe kutoka kwenye vumbi na kufanywa kiumbe cha Mungu, lakini pia aliweza kumteketeza mwanadamu kwa moto, na kumlaani mwanadamu kwa kutumia kiboko Chake ili kutawala mwanadamu. Kwa hivyo, wao pia, waliweza kuona kwamba Yehova angeweza kuyaongoza maisha ya binadamu ulimwenguni na kuongea na kufanya kazi miongoni mwao mchana na usiku. Alifanya tu kazi hiyo ili viumbe Vyake viweze kujua kwamba binadamu alitoka kwenye vumbi na akachukuliwa na Yeye, kwamba binadamu aliumbwa na Yeye. Aidha, kazi Aliyoianza Israeli ilikuwepo ili watu wengine na mataifa mengine (ambao kwa hakika hawakuwa kando na wale wa Isreali, lakini walikuwa wamejitenga na wana wa Israeli, ilhali bado walikuwa kizazi cha Adamu na Hawa) waweze kupokea injili ya Yehova kutoka Israeli, ili viumbe vyote ulimwenguni vingemstahi na kumchukulia kuwa mkuu. Kama Yehova Asingekuwa Ameanza kazi yake Israeli, lakini badala yake baada ya kumwumba mwanadamu, na kumwacha kuishi vivyo hivyo tu hapa ulimwenguni, basi kwa sababu ya asili ya kimaumbile ya binadamu (asili inamaanisha kwamba binadamu hawezi kujua yale mambo ambayo hayaoni, yaani, hajui kwamba Yehova Alimwumba mwanadamu, na vilevile hata hajui kwa nini Alifanya hivyo), asingewahi kujua kwamba Yehova Alimwumba mwanadamu na kwamba ndiye Bwana wa mambo yote. Kama Yehova Angemwumba mwanadamu na kumweka ulimwenguni kwa raha Zake, kisha kuikung’uta tu mikono Yake na kuondoka badala ya kumwongoza miongoni mwa wenzake kwa kipindi cha muda, basi kizazi chote cha binadamu kingerudi katika hali ya kutokuwa na maana; hata mbingu na ardhi na vitu vyote vilivyoumbwa na Yeye, ukiwemo ubinadamu wote, vingerudi na kuwa katika hali isiyokuwa na maana na kutupiliwa mbali na kukanyagwa na Shetani. Na kwa hivyo, mapenzi ya Yehova kwamba “Anafaa kuwa na mahali pa kusimama hapa ulimwenguni, mahali patakatifu miongoni mwa viumbe Vyake” yasingetimia. Kwa hiyo badala yake, baada ya Mungu kuumba wanadamu Aliwaongoza katika maisha yao na kuwazungumzia, wote ili waweze kutambua matamanio yake, kufikia mpango Wake. Kazi ya Mungu nchini Israeli ilinuiwa kutekeleza kazi Aliyokuwa Ameiweka wazi mbele ya viumbe Vyake vyote, na kwa hivyo Yeye kufanya kazi kwanza miongoni mwa Waisraeli na viumbe Wake kati ya vitu vyote havikuwa katika mgongano, lakini vyote hivi vilikuwa kwa minajili ya usimamizi Wake, kazi Yake na utukufu Wake, na kuzidisha maana ya kuumba Kwake wanadamu. Aliyaongoza maisha ya wanadamu ulimwenguni kwa miaka elfu mbili baada ya Nuhu ambapo Aliwafunza namna ya kustahi Yehova Bwana wa vitu vyote, Akawafunza namna ya kujiendeleza na kuisha maisha yao, na muhimu kuliko vyote, namna ya kuwa shahidi wa Yehova, kumtii Yeye na kumstahi Yeye, na kumsifu Yeye kwa muziki kama Daudi na kuhani wake walivyofanya.
Kabla ya miaka hiyo elfu mbili ambayo Yehova Alifanya kazi Yake, binadamu hakujua chochote na karibu kila kitu kilizoreteka na kugeuka kuwa uasherati na upotovu vyote ambavyo vilitangulia mafuriko; mioyo yao haikuwa na nafasi yoyote ya Yehova, wala hata njia Yake. Hawakuwahi kuelewa kazi ambayo Yehova Alikuwa Akienda kufanya; walikosa akili, na hata maarifa, kama vile mitambo inayoishi na kupumua, kutojua binadamu, Mungu, ulimwengu, na maisha vilevile. Ulimwenguni walijihusisha na kupotoka kwingi kama alivyofanya yule nyoka, na kusema mambo mengi ambayo yalimchukiza Yehova, lakini kwa sababu hawakujua lolote, Yehova hakuwaadibu wala kuwafundisha nidhamu. Baada ya mafuriko wakati Nuhu alikuwa na umri wa miaka 601, Yehova Alijionyesha rasmi kwa Nuhu na Akamwongoza yeye na familia yake, Akamwongoza yeye, ndege, na wanyama walionusurika mafuriko na vizazi vyake mpaka mwisho wa Enzi ya Sheria, jumla ya miaka 2,500. Alikuwa rasmi kazini nchini Israeli kwa miaka 2,000, na kipindi ambacho Alikuwa kazini nchini Israeli na nje ya Israeli kilikuwa miaka 500, kwa hivyo kwa pamoja ni miaka 2,500. Kwenye kipindi hiki Aliwaagiza Waisraeli kwamba ili kuweza kumhudumia Yehova, wanafaa kujenga hekalu na kuvalia majoho ya kikuhani, kutembea bila viatu kwenye hekalu wakati wa mapambazuko, na kama wasingefanya hivyo viatu vyao vingechafua hekalu na moto ungetumwa chini kwao kutoka paa la hekalu na kuwateketeza hadi kifo. Walitekeleza wajibu wao na kutii mipango ya Yehova. Walimwomba Yehova hekaluni, na baada ya huhamasishwa na Yehova, yaani baada ya Yehova kuongea, waliwaongoza watu na kuwafunza kwamba wanafaa kumstahi Yehova—Mungu wao. Na Yehova Aliwafunza kwamba wanafaa kulijenga hekalu na madhabahu, na kwa wakati uliotengwa na Yehova, yani, kwenye msimu wa Pasaka, wanafaa kutayarisha ndama na wanakondoo wachanga kwenye madhabahu kama dhabihu ili kuhudumia Yehova ili kuwazuia wao na kuweza kumstahi Yehova katika mioyo yao. Kama wangetii sheria hii ndicho kingekuwa kipimo cha uaminifu wao kwa Yehova. Yehova pia Aliwatengea siku ya Sabato, siku ya saba ya kuumba Kwake. Siku moja baada ya hiyo, Alifanya siku ya kwanza, siku ya wao kusifu Yehova, kumpa Yehova dhabihu na kumchezea muziki Yehova. Kwenye siku hii, Yehova Aliwaita makuhani wote na kugawanya dhabihu hizo kwenye madhabahu ili watu waweze kula na kufurahia kafara zilizotolewa kwa Yehova. Naye Yehova Akasema kwamba walikuwa wamebarikiwa na walikuwa na sehemu Yake, na kwamba walikuwa ndio watu Wake waliochaguliwa (ambalo ndilo lililokuwa agano la Yehova na wana wa Israeli) Na ndiyo maana, mpaka siku hii watu wa Israeli wangali wanasema kwamba Yehova ndiye Mungu wao pekee na wala si Mungu wa watu wengine.
Kwenye Enzi ya Sheria, Yehova Aliweza kuweka wazi sheria nyingi kwa Musa kupitisha kwa wana wa Israeli waliomfuata kutoka Misri. Yehova Aliwakabidhi sheria hizi wana wa Israeli ambazo hazikuwa na uhusiano wowote na Wamisri, na zilinuiwa kuwazuia wana wa Israeli, na ndiyo yaliyokuwa mahitaji Yake kwao. Kama mtu alitii sheria ya Sabato, kama mtu aliheshimu wazazi wake, kama mtu aliabudu miungu na kadhalika, hizi ndizo zilizokuwa kanuni ambazo mtu alihukumiwa na kujulikana kama mwenye dhambi au mwenye haki. Kama mtu alichomwa na moto wa Yehova, au kupigwa na mawe hadi kufa, au kupokea baraka za Yehova, vyote hivi viliamuliwa kulingana na kama mtu alitii sheria hizi. Wale ambao hawakutilia maanani Sabato walipigwa mawe hadi kufa. Wale kuhani ambao hawakutilia maanani Sabato waliteketezwa na moto wa Yehova. Wale hawakuheshimu wazazi wao waliweza kupigwa mawe pia hadi kufa. Haya yote yalishauriwa na Yehova. Yehova Alianzisha sheria Zake na taratibu ili huku Akiyaongoza maisha yao, watu wangeweza kumsikiliza na kuheshimu neno Lake na wala si kuasi neno Lake. Alitumia sheria hizi kuweza kudhibiti kizazi kipya cha binadamu kilichozaliwa, kuweka msingi wa kazi Yake ambayo ingefuata. Na kwa hivyo, sababu ya kazi ambayo Yehova Alifanya, enzi ya kwanza iliitwa Enzi ya Sheria. Ingawaje Yehova Aliongea sana na Alifanya kazi nyingi, Aliwaongoza tu kwa njia nzuri huku Akiwafunza watu hawa wasiojua namna ya kuwa na wema, namna ya kuishi, namna ya kuelewa njia ya Yehova. Katika sehemu kubwa ya kazi Yake kwa hakika Alinuia kuruhusu watu Wake kufuatilia njia Yake na kufuata sheria Yake. Kazi ilifanyiwa watu ambao walikuwa wamepotoka kidogo; haikujali sana mageuzi ya tabia au ukuzi wa maisha. Alijali tu matumizi ya sheria ya kuzuia na kudhibiti watu. Kwa wana wa Israeli wakati huo, Yehova Alikuwa tu Mungu kwenye hekalu, Mungu kwenye mbingu. Alikuwa mnara wa wingu, mnara wa moto. Kile ambacho Yehova Aliwahitaji kufanya kilikuwa ni kutii kile ambacho watu wanajua leo kama sheria na mafundisho Yake—mtu angeweza hata kusema taratibu—kwa sababu kazi ya Yehova haikunuiwa kuwabadilisha, lakini kuwapatia vitu vingi ambavyo binadamu anastahili kuwa navyo, kuwaambia kutoka kwenye kinywa Chake mwenyewe, kwa sababu baada ya binadanu kuumbwa, binadamu hakujua chochote kuhusu kile alichostahili kumiliki. Na kwa hivyo Yehova Aliwapatia vitu walivyostahili kumiliki katika maisha yao hapa ulimwenguni, Akawafanya watu Aliokuwa Amewaongoza kuzidi vizazi vyao, Adamu na Hawa, kwa sababu kile Yehova Alichowapatia kilizidi kile Alichokuwa Amepatia Adamu na Hawa hapo mwanzo. Licha ya hayo yote, kazi ambayo Yehova Alifanya Israeli ilikuwa tu kuongoza kizazi cha binadamu na kukifanya kutambua Mungu wao. Hakuwashinda wala kuwabadilisha, Aliwaongoza tu. Hii ndiyo jumla ya kazi ya Yehova kwenye Enzi ya Sheria. Ndiyo maelezo ya ziada, hadithi ya kweli, kiini cha kazi Yake kwenye nchi nzima ya Israeli na mwanzo wa kazi Yake ya miaka elfu sita—katika kudhibiti mwanadamu kwa mkono wa Yehova. Kutokana na haya yote kazi nyingi zaidi ilijitokeza kwenye mpango Wake wa usimamizi wa miaka-elfu-sita.
kutoka kwa Neno Laonekana Katika Mwili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni