Jumatatu, 6 Agosti 2018

Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wokovu

         Mabadiliko ya Mtu Aliyeanguka

       Tong Xin    Mkoa wa Fujian
Nilizaliwa vijijini. Nilitoka kwa nasaba ya wakulima wanyenyekevu na zaidi ya hayo familia yetu ilikuwa na watu wachache, kwa hiyo mara nyingi tulikuwa tunadhulumiwa. Nilipokuwa na umri wa miaka 13, kulikuwa na mtoto aliyepigwa na mtu fulani kutoka nje ya kijiji chetu. Wanakijiji walimlaumu kwa uongo baba yangu kwa kuchochea hilo na wakasema walitaka kupekua nyumba yetu na kuchukua ngawira mali yetu, kuchukua nguruwe wetu na hata kumpiga baba yangu. Kulikuwa na wakati pia ambapo mwanakijiji mwingine alichukua wavu wetu wa uvuvi na kuuweka kama wake mwenyewe.

Jumapili, 5 Agosti 2018

Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Tisa

Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Tisa

Inaonekana kwamba katika mawazo ya watu, Mungu ni wa fahari sana naye Haeleweki. Ni kana kwamba Mungu haishi miongoni mwa wanadamu, kana kwamba anawadharau watu kwa sababu Yeye ni wa fahari sana. Mungu, hata hivyo, Huziseta fikira za wanadamu na kuzifuta zote, Akizika fikira zao zote ndani ya "makaburi" ambamo zinageuka kuwa majivu. Mtazamo wa Mungu kwa fikira za wanadamu ni sawa na mtazamo Wake kwa wafu, Akiwafafanua apendavyo. Ni kana kwamba hakuna athari kutokana na fikira. Kwa hiyo tangu uumbaji wa ulimwnegu mpaka sasa, Mungu amekuwa Akifanya kazi hii na Hajaacha kamwe. Kwa sababu ya mwili, wanadamu hupotoshwa na Shetani, na kwa sababu ya matendo ya Shetani duniani, wanadamu huunda kila aina ya fikira wakati wa uzoefu wao.

Jumamosi, 4 Agosti 2018

Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Saba

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Saba

Kwa kweli, maneno yote kutoka katika kinywa cha Mungu ni mambo ambayo wanadamu hawayajui; yote ni lugha ambayo watu hawajasikia, kwa hiyo inaweza kusemwa hivi: Maneno ya Mungu yenyewe ni siri. Watu wengi kwa kutojua wanaamini kwamba ni mambo tu ambayo watu hawawezi kutimiza kimawazo, mambo ya mbinguni ambayo Mungu anawawezesha watu kuyajua sasa, au ukweli kuhusu kile Mungu anachofanya katika ulimwengu wa kiroho ni siri.

Ijumaa, 3 Agosti 2018

Tamko la Arubaini na Sita

Sijui jinsi watu wanavyoendelea katika kuyafanya maneno Yangu kuwa msingi wa kuweko kwao. Nimehisi wasiwasi kila mara kwa ajili ya majaliwa ya mwanadamu, lakini watu hawaonekani kuwa na fahamu yoyote kuhusu hili—na kutokana na hilo, hawajawahi kuyatilia maanani mambo Yangu, na hawajawahi kukuza kuabudu kokote kwa ajili ya mtazamo Wangu kuhusiana na mwanadamu. Ni kana kwamba walitupa hisia zamani ili kuuridhisha moyo Wangu. Nikikumbwa na hali kama hizo, Nakimya mara nyingine.

Jumapili, 29 Julai 2018

Kuzishika Amri na Kuutenda Ukweli


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kuzishika Amri na Kuutenda Ukweli

Katika matendo, amri zapaswa kuunganishwa na matendo ya ukweli. Wakati unapozishika amri, mtu anapaswa kutenda ukweli. Wakati anapotenda ukweli, mtu hapaswi kukiuka kanuni za amri au kwenda kinyume na amri. Fanya yale ambayo Mungu anahitaji uyafanye. Kuzishika amri na kuutenda ukweli vinahusiana, bali havikinzani. Zaidi unavyotenda ukweli, ndivyo unavyoweza kutilia maanani zaidi kiini cha amri. Zaidi unavyotenda ukweli, ndivyo utakavyoweza kulielewa zaidi neno la Mungu kama ilivyoonyeshwa katika amri.

Jumapili, 15 Julai 2018

Tamko la Pili

Kufuata kuanza kazi kwa mtazamo mpya, kutakuwa na hatua mpya katika kazi Yangu. Kama ilivyo katika ufalme, Nitafanya mambo moja kwa moja kupitia kwa uungu, Nikiongoza kila hatua ya njia, sahihi hadi kwa maelezo madogo, na bila kutiwa najisi na nia za binadamu hata kidogo. Yafuatayo yanaeleza kwa muhtasari namna ya utekelezaji halisi: Kwa vile ni kupitia katika ugumu na usafishaji ndiyo wamepata jina la “watu”, na kama walivyo watu wa ufalme Wangu, lazima Niwafanye watii kwa mahitaji kali, ambayo ni ya juu kushinda mbinu za kazi Yangu kwa vizazi vilivyopita.

Jumamosi, 14 Julai 2018

Tamko la Kwanza

Tamko la Kwanza

Je, wale wanaoshuhudia maneno Yangu huyakubali kwa kweli? Je, mnanijua kwa kweli? Mmejifunza utiifu kweli? Ninyi hutumia rasilimali kwa ajili Yangu kwa uaminifu? Mmekuwa na ushuhuda thabiti, usiokubali kushindwa Kwangu mlipokabiliwa na joka kuu jekundu? Je, moyo wenu wa ibada hulifedhehesha kweli joka kuu jekundu? Ni kupitia tu kwa jaribio la maneno Yangu ndipo Naweza kutimiza lengo Langu la kulitakasa kanisa na kuwachagua wale wanaonipenda Mimi kweli.

Jumanne, 10 Julai 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Dibaji

Ingawa watu wengi wanaamini katika Mungu, ni wachache wanaoelewa ni nini maana ya imani katika Mungu, na ni nini wanachopaswa kufanya ili waupendeze moyo wa Mungu. Hii ni kwa sababu, hata ingawa watu wengi wanalifahamu neno “Mungu” na mafungu ya maneno kama “kazi ya Mungu”, hawamjui Mungu, sembuse kujua kazi ya Mungu. Si ajabu, basi, kwamba wale wote wasiomjua Mungu wamejawa na imani iliyovurugika. Watu hawachukulii imani kwa Mungu kwa uzito kwa kuwa kuamini Mungu ni jambo geni, jambo lisilo la kawaida sana kwao. Kwa njia hii, hawafikii mahitaji ya Mungu.

Jumatatu, 9 Julai 2018

Swahili Worship Song "Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu" | Seeing the Love of God

Swahili Worship Song "Unapoufungua Moyo Wako kwa Mungu" | Seeing the Love of God
Wakati hamumwelewi Mungu na hamjui asili Yake,

mioyo yenu haiwezi kamwe kufunguka, kufunguka kwa Mungu.

Mara utakapomwelewa Mungu wako,

utaelewa kile kilicho moyoni Mwake,

na kufurahia kile kilicho ndani Yake

kwa imani na usikivu wako wote.

Jumamosi, 7 Julai 2018

Tamko la Kwanza

Tamko la Kwanza

Sifa zimekuja Uyahudi na makazi ya Mungu yameonekana. Jina tukufu takatifu linasifiwa na watu wote, na linaenea. Ah, Mwenyezi Mungu! Mkuu wa ulimwengu, Kristo wa siku za mwisho—Yeye ni Jua linalong’aa, na Ameinuka juu ya Mlima Sayuni ulio na uadhimu na mzuri kabisa katika ulimwengu mzima ...

Ijumaa, 6 Julai 2018

Tamko la Hamsini

Tamko la Hamsini

Makanisa yote na watakatifu wote wanapaswa kutafakari kuhusu siku zilizopita na kutumainia siku za usoni: Ni mangapi kati ya matendo yenu ya zamani ndiyo yanayostahili, na ni mangapi kati yao yalishiriki katika ujenzi wa ufalme? Usiwe mtu mwenye kujifanya kujua kila kitu! Unapaswa kuona wazi dosari zako na unafaa kuelewa hali zako mwenyewe.

Jumapili, 1 Julai 2018

Utangulizi

Utangulizi

"Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima" ni matamshi yanayoonyeshwa na Kristo, ambayo kwayo Anatumia utambulisho wa Mungu Mwenyewe. Yanajumlisha kipindi cha kuanzia Februari 20, 1992 hadi Juni 1, 1992, na yana jumla ya matamshi arobaini na saba. Katika fungu hili la matamshi, Mungu anaonyesha maneno Yake kutoka kwa mtazamo wa Roho. Namna ambayo Anazungumza haiwezi kufikiwa na wanadamu walioumbwa.