Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Roho Mtakatifu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Roho Mtakatifu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 11 Novemba 2018

Filamu za Kikristo 2018 | "Kumbukumbu Chungu" | Welcoming the Return of the Lord in Judgement



Fan Guoyi alikuwa mzee wa kanisa la nyumba kule Uchina. Wakati wa zaidi ya miaka ishirini ya huduma, siku zote alimwiga Paulo, na kufanya kazi kwa bidii na akamtumikia Bwana kwa shauku kubwa. Aidha, alisadiki kabisa kwamba katika kufuata imani yake kwa njia hii, alikuwa akitenda mapenzi ya Baba wa mbinguni, na kwamba wakati Bwana angerudi, angenyakuliwa kwa hakika na kuenda kwenye ufalme wa mbinguni. 

Jumanne, 6 Novemba 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Kumi na Mbili

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Tamko la Kumi na Mbili


Ikiwa una tabia ambayo si thabiti, nyepesi kuhamaki kama upepo au mvua, kama huwezi kuendelea kusonga mbele, basi fimbo Yangu haitakuwa mbali na wewe. Unaposhughulikiwa, kadiri hali ilivyo mbaya zaidi, na kadiri unavyoteswa zaidi, ndivyo upendo wako kwa Mungu unavyoongezeka, na unaacha kushikilia dunia. Bila njia nyingine, unakuja Kwangu, na unapata tena nguvu na imani yako. Ilhali, katika hali rahisi, ungeboronga. Ni lazima uingie ndani kwa mtazamo chanya, uwe mwenye vitendo na si baridi. Hutatingisika na yeyote na chochote katika hali yoyote, na huwezi kushawishiwa na maneno ya yeyote.

Jumapili, 28 Oktoba 2018

Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje


Uhusiano Wako Na Mungu Ukoje



Mwenyezi Mungu anasema, "Katika kuwa na imani kwa Mungu, ni lazima angalau utatue swala la kuwa na uhusiano wa kawaida na Mungu. Bila uhusiano wa kawaida na Mungu, basi umuhimu wa kumwamini Mungu unapotea. Kuunda uhusiano wa kawaida na Mungu kunapatikana kikamilifu kupitia kuutuliza moyo wako mbele ya Mungu.

Jumapili, 14 Oktoba 2018

Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu (Sehemu ya Kwanza)


Smiley face


Ni kiasi gani cha kazi ya mwanadamu ni kazi ya Roho Mtakatifu na uzoefu wa mwanadamu ni kiasi gani? Hata sasa, tunaweza kusema kuwa watu bado hawayaelewi maswali haya, ambayo yote ni kwa sababu watu hawaelewi kanuni za utendaji kazi wa Roho Mtakatifu. Kazi ya mwanadamu Ninayoizungumzia, kimsingi, ni kwa kurejelea kazi za wale ambao wana kazi ya Roho Mtakatifu au wale ambao wanatumiwa na Roho Mtakatifu.

Alhamisi, 27 Septemba 2018

Uchaguzi Kutoka katika Mafungu Kumi ya Neno la Mungu juu ya "Kuhusu Biblia"

Mwenyezi Mungu, Biblia, Bwana Yesu,

Uchaguzi Kutoka katika Mafungu Kumi ya Neno la Mungu juu ya "Kuhusu Biblia"

1. Kwa miaka mingi, imani ya watu ya kitamaduni (hiyo ya Ukristo, moja ya dini kuu tatu za dunia) imekuwa ni kusoma Biblia; kujitenga na Biblia sio imani kwa Bwana, kujitenga na Biblia ni madhehebu maovu, na uzushi, na hata pale watu wanaposoma vitabu vingine, msingi wa vitabu hivi ni lazima uwe ni ufafanuzi wa Biblia. Ni kusema kwamba, kama unasema unamwamini Bwana, basi ni lazima usome Biblia, unapaswa kula na kunywa Biblia, na nje ya Biblia hupaswi kuabudu kitabu kingine ambacho hakihusishi Biblia.

"Sauti Nzuri Ajabu" (2) - Tunawezaje Kuwa na Uhakika kuwa Bwana Yesu Tayari Amerudi?


Tangu makanisa yalipoanza kukumbwa na ukiwa, ndugu wengi katika Bwana wamehisi kwa uwazi ukosefu wa kazi ya Roho Mtakatifu na uwepo wa Bwana, na wote wanatamani kurudi kwa Bwana. Lakini wakati tunaposikia habari ya kwamba Bwana Yesu tayari amerudi, tunawezaje kuwa na uhakika wa hili?

Sikiliza zaidi: Asili ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 18 Septemba 2018

Neno la Mungu "Jinsi ya Kuujua Uhalisi"


Mwenyezi Mungu alivyosema, "Mungu ni Mungu wa uhalisi: kazi Zake zote ni halisi, maneno yote Anayoyanena ni halisi, na ukweli wote Anaouonyesha ni halisi. Kila kisicho maneno Yake ni kitupu, kisichokuwepo, na kisicho timamu. Leo, Roho Mtakatifu yupo kwa ajili ya kuwaongoza watu katika maneno ya Mungu. Ikiwa watu wanatafuta kuingia katika uhalisi, basi ni lazima wauandame uhalisi, na waujue uhalisi, baadaye ni lazima wapitie uhalisi, na kuishi kwa kudhihirisha uhalisi.

Worship and Praise Dance | "Wale Wanaompenda Mungu kwa Dhati Wote ni Watu Waaminifu" (Swahili Sub)


Safi na mwaminifu kama mtoto, asiye na hatia na mchangamfu, aliyejawa na nguvu za ujana,
wao ni kama malaika wanaokuja ulimwenguni.
Hakuna uongo, udanganyifu au hadaa, na moyo ulio wazi na mwaminifu, wanaishi na heshima.
Wanaitoa mioyo yao kwa Mungu, Mungu anawaamini, na wao ni watu waaminifu ambao Mungu anapenda.
Wale wanaopenda ukweli wote wana mioyo ya uaminifu.
Watu waaminifu hufurahia kutenda ukweli, na kwa kumtii Mungu mioyo yao ina amani.

Jumapili, 12 Agosti 2018

Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Umeme wa Mashariki, mapenzi ya Mungu, Ukweli

Kupitia Upendo Maalum wa Mungu

Jiayi     Mji wa Fuyang, Mkoa wa Anhuif
Asili yangu ni ya kiburi hasa; bila kujali ninafanya nini, mimi daima hutumia werevu na ujuzi wa kubuni ili kuonyesha akili yangu na kwa hiyo mara kwa mara hukiuka mipango ya kazi ili nifanye mambo kwa njia yangu mwenyewe. Mimi ni mwenye kiburi hasa kuhusu kuchagua watu kwa cheo fulani. Ninaamini kuwa nina talanta ya kipekee na umaizi ambavyo hunisaidia daima kumchagua mtu sahihi. Kwa sababu ya hili, nilipomchagua mtu, singechunguza kwa dhati ili kuelewa hali zote za mtu niliyetaka kumchagua. Pia singewapima kwa makini watu ambao ninataka kuchagua kulingana na maadili yanayohusiana.