Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo majaribio. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo majaribio. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 24 Agosti 2018

Ufafanuzi wa Tamko la Arubaini na Sita

Mwenyezi Mungu, ushuhuda , majaribio

Ufafanuzi wa Tamko la Arubaini na Sita

Miongoni mwa maneno haya yote, hakuna yasiyoweza kusahaulika zaidi kama yale ya leo. Awali maneno ya Mungu yalifichua hali za mwanadamu au siri za mbinguni, lakini tamko hili halifanani na yale ya wakati uliopita. Halidhihaki wala kufanya mzaha, lakini ni kitu kisichotarajiwa kabisa: Mungu aliketi chini na Akazungumza na watu kwa utulivu. Kusudi Lake ni gani? Unaona nini Mungu anaposema, “Leo, Nimeanza kazi mpya juu ya ulimwengu. Nimewapa watu walio duniani mwanzo mpya, na Nimewaambia wote watoke nyumbani Mwangu. Na kwa kuwa kila mara watu hupenda kujideka, Nawashauri wajijue, na wasiisumbue kazi Yangu kila mara”? Ni huu "mwanzo mpya" ambao Mungu anazungumzia ni upi?

Ijumaa, 1 Juni 2018

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | Wale Waliofanywa Kuwa Watimilifu Ndio Tu Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

Mwenyezi Mungu,Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | Wale Waliofanywa Kuwa Watimilifu Ndio Tu Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa kweli, kazi inayofanywa sasa ni kuwafanya watu kumtoroka Shetani, kutoroka babu zao wa kale. Hukumu zote kwa neno zinalenga kufichua tabia potovu ya binadamu na kuwawezesha watu kuelewa kiini cha maisha. Hukumu hizi zote zilizorudiwa zinapenyeza mioyo ya watu. Kila hukumu inaathiri kwa njia ya moja kwa moja hatima yao na inalenga kujeruhi mioyo yao ili waweze kuachilia yale mambo yote husika na hivyo basi kuja kujua maisha, kuujua ulimwengu huu mchafu, na pia kujua hekima ya Mungu na uweza Wake na kujua mwanadamu huyu aliyepotoshwa na Shetani.

Alhamisi, 17 Mei 2018

Zawadi ya Kupendeza Zaidi Ambayo Mungu Amenipa

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,mkristo

Zawadi ya Kupendeza Zaidi Ambayo Mungu Amenipa
Yixin    Jiji la Shijiazhuang, Mkoa wa Hebei
Kabla, ningewasikia mara kwa mara ndugu zangu wa kiume na wa kike wakisema, "Kila kitu ambacho Mungu hufanya ni kwa ajili ya matokeo mazuri; ndiyo yote wanayohitaji watu." Nilikubali hili na kukubaliana nalo, lakini sikuwa na ufahamu wowote kupitia uzoefu wangu mwenyewe. Baadaye nilipata ufahamu kiasi kwa njia ya mazingira ambayo Mungu aliniumbia.

Jumamosi, 10 Februari 2018

Swahili Gospel Video "Kanisa la Nafsi Tatu ni Mwavuli Wangu"

Utambulisho

Wakati mmoja, serikali ya Kikomunisti ya Uchina iliwakamata Wakristo wengi wa Kanisa la Mwenyezi Mungu kutoka mahali fulani usiku wa manane. Jambo hili lilisababisha ghasia kubwa mahali hapo. Lilichochea majadiliano miongoni mwa washirika wa Kanisa la Nafsi Tatu. Watu wengine waliamini kwamba Umeme wa Mashariki umepitia ukandamizaji na mateso ya kikatili ya serikali ya kikomunisti ya Uchina. Ni hatari sana kuamini katika Umeme wa Mashariki, na ni salama sana kuamini katika Kanisa la Nafsi Tatu. Hawatapitia taabu na wataweza kuingia katika ufalme wa mbinguni.

Jumatano, 7 Februari 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Tamko La Thelathini na Mbili

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,ndugu na dada

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Tamko La Thelathini na Mbili

Watu wanapokusanyika pamoja na Mimi, moyo Wangu unajawa na furaha. Mara moja, Ninatoa baraka zilizo mkononi Mwangu miongoni mwa binadamu, ili watu waweze kukusanyika kwa mkutano na Mimi, na kutokuwa maadui wanaoniasi lakini marafiki wanaotangamana na Mimi. Hivyo, Mimi pia ni wa dhati kwa mwanadamu.

Jumatano, 31 Januari 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Ufafanuzi wa Tamko la Sita

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,uaminifu

Kanisa la Mwenyezi Mungu|Ufafanuzi wa Tamko la Sita

Binadamu wanapigwa bumbuazi kwa sababu ya matamshi ya Mungu wanapotambua kwamba Mungu amefanya kitendo kikubwa katika ulimwengu wa kiroho, kitu ambacho mwanadamu hawezi na ambacho Mungu Mwenyewe pekee ndiye Anaweza kufanikisha. Kwa sababu hii, Mungu mara tena anawasilisha maneno ya huruma kwa wanadamu. Mioyo ya watu inapojaa ukinzani, ikishangaa: “Mungu ni Mungu asiye na huruma au upendo, lakini badala yake Mungu aliyejitolea kuwaangusha binadamu; kwa hiyo mbona Atuonyeshe huruma?