 |
hukumu,ushahidi |
Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo|3.Baada ya Kupoteza Hadhi Yangu
Huimin Mji wa Jiaozuo, Mkoa wa Henan
Kila wakati nilipoona au kusikia kuhusu mtu aliyekuwa amebadilishwa naye kujisikia mwenye huzuni, dhaifu au mnunaji, na kutotaka kufuata tena, basi niliwaangalia kwa dharau. Nilidhani haikuwa kitu zaidi ya watu tofauti waliokuwa na majukumu tofauti ndani ya
kanisa, kwamba hakukuwa na tofauti kati ya juu au chini, kwamba sote tulikuwa uumbaji wa
Mungu na hakukuwa na sababu ya kuhuzunikia.