Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Roho-Mtakatifu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Roho-Mtakatifu. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 13 Julai 2019

Neno la Mungu | Sura ya 96


Nitamwadibu kila mtu aliyezaliwa kutoka Kwangu ambaye bado hanijui ili kuonyesha ghadhabu Yangu yote, kuonyesha nguvu Zangu kuu, na kuonyesha hekima Yangu kamili. Ndani Yangu kila kitu ni chenye haki na bila shaka hakuna udhalimu, hakuna udanganyifu, na hakuna upotovu; yeyote ambaye ni mpotovu na mdanganyifu lazima awe ni mwana wa jahanamu—lazima amezaliwa huko kuzimu. Ndani Yangu kila kitu ni cha wazi; chochote Ninachosema kukamilisha kinakamilika na chochote Ninachosema kuanzisha kinaanzishwa, na hakuna mtu anayeweza kubadilisha au kuiga mambo haya kwa sababu Mimi ndimi Mungu Mwenyewe wa pekee. 

Ijumaa, 5 Julai 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya ‘Wingu Jeupe’”




Maneno ya Roho Mtakatifu kwa makanisa | “Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya ‘Wingu Jeupe’”


Mwenyezi Mungu anasema, “Tangu Yesu aondoke, wafuasi waliomfuata, na watakatifu wote waliookolewa kwa sababu ya jina Lake, wamekuwa wakimtamani mno na kumngoja. Wale wote waliookolewa kwa neema ya Yesu Kristo katika Enzi ya Neema wamekuwa wakiitamani siku hiyo ya furaha katika siku za mwisho, wakati ambapo Yesu Mwokozi atawasili juu ya wingu jeupe na kuonekana kati ya mwanadamu. Bila shaka, haya pia ni mapenzi ya pamoja ya wale wote wanaolikubali jina la Yesu Mwokozi leo.

Jumatano, 26 Juni 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako”



Maneno ya Roho Mtakatifu | “Unapaswa Kutayarisha Matendo Mema ya Kutosha kwa ajili ya Hatima Yako”

Mwenyezi Mungu anasema, “Huruma Zangu zinaonyeshwa kwa wale wanaonipenda Mimi na kujinyima wenyewe. Na adhabu inayoletwa kwa waovu ni thibitisho hasa la tabia Yangu ya haki na, zaidi sana, ushuhuda wa hasira Yangu. Msiba utakapokuja, njaa na baa litawakumba wale wote wanaopinga Mimi na watalia kwa uchungu. Wale wote ambao wametenda aina zote za uovu, lakini ambao wamenifuata kwa miaka mingi, hawataepuka shtaka rasmi lililoandikwa; wao pia, wakijipata katika maafa, ambayo yameonekana kwa nadra katika enzi zote, wataishi katika hali ya kila siku ya taharuki na woga. 

Jumatatu, 24 Juni 2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 86


Watu husema kuwa Mimi ni Mungu mwenye huruma na wao husema kwamba Nitaoa wokovu kwa kila kitu Nilichokiumba—mambo haya yote yanasemwa kulingana na fikira za binadamu. Kunitaja Mimi kama Mungu mwenye huruma kunaelekezewa wazaliwa Wangu wa kwanza na kuletea Kwangu wokovu kunaelekezewa wazaliwa Wangu wa kwanza na watu Wangu. Kwa sababu Mimi ni Mungu mwenye hekima, ni wazi katika mawazo Yangu ni nani Ninaowapenda na ni nani Ninaowachukia. 

Jumatano, 22 Mei 2019

Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”



Neno la Mungu | “Mwanadamu Mpotovu Hawezi Kumwakilisha Mungu”


      Mwenyezi Mungu anasema, “Vitendo vyote na matendo ya Shetani vinaonyeshwa kupitia kwa binadamu. Sasa vitendo vyote na matendo yote ya binadamu ni maonyesho ya Shetani na hivyo basi haviwezi kumwakilisha Mungu. Binadamu ni mfano halisi wa Shetani, na tabia ya mwanadamu haiwezi kuiwakilisha tabia ya Mungu. Baadhi ya wanadamu ni wenye tabia nzuri; Mungu anaweza kufanya baadhi ya kazi kupitia kwa tabia hiyo nayo kazi yao inatawaliwa na Roho Mtakatifu. 

Jumanne, 7 Mei 2019

Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza



Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | “Mungu na Mwanadamu Wataingia Rahani Pamoja” sehemu ya kwanza


      Mwenyezi Mungu anasema, "Kuingia rahani hakumaanishi kwamba mambo yote yatakoma kusonga, ama kwamba mambo yote yatakoma kuendelea, wala hakumaanishi kwamba Mungu atakoma kufanya kazi ama mwanadamu atakoma kuishi. Ishara ya kuingia rahani ni kama hii: Shetani ameangamizwa; wale watu waovu wanaomuunga mkono Shetani kwa kufanya maovu wameadhibiwa na kuondolewa; nguvu zote za uhasama kwa Mungu zimekoma kuwepo.

Jumatatu, 29 Aprili 2019

Matamshi ya Roho Mtakatifu | "Mazungumzo Mafupi Kuhusu 'Ufalme wa Milenia Umefika'"


Matamshi ya Roho Mtakatifu | "Mazungumzo Mafupi Kuhusu 'Ufalme wa Milenia Umefika'"


Mwenyezi Mungu anasema, "Wakati wa Enzi ya Ufalme wa Milenia, watu tayari watakuwa wamefanywa wakamilifu, na tabia mbovu ndani yao zitakuwa zimetakaswa. Wakati huo, maneno yasemwayo na Mungu yatawaongoza wanadamu hatua kwa hatua, na kufichua siri za kazi ya Mungu tangu uumbaji hadi leo, na maneno Yake yatawaambia watu kuhusu matendo ya Mungu katika kila enzi na kila siku, jinsi Anavyowaongoza watu ndani, kazi Aifanyayo katika ufalme wa kiroho, na yatawaambia watu kuhusu mienendo ya ufalme wa kiroho. Hapo tu ndipo itakuwa Enzi ya kikweli ya Neno; kwa sasa ni mfano tu."

Jumatano, 17 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 62


Mwenyezi Mungu anasema, “Kuyaelewa mapenzi Yangu hakufanywi ili tu kwamba uweze kujua, ila pia kwamba uweze kutenda kulingana na nia Yangu. Watu hawauelewi moyo Wangu. Ninaposema huku ni mashariki, wanalazimika kuenda na kutafakari, wakijiuliza, “Kweli ni mashariki? Pengine sio. Siwezi kuamini kwa urahisi hivyo. Nahitaji kujionea mwenyewe.” Ninyi watu ni wagumu sana kushughulikia, na hamjui utii wa kweli ni nini.

Jumanne, 16 Aprili 2019

Neno la Mwenyezi Mungu | Sura ya 61


Mwenyezi Mungu anasema, “Ukiwa na ufahamu wa hali yako mwenyewe basi utafanikisha mapenzi Yangu. Kwa kweli, mapenzi Yangu si magumu kushika, ni kwamba tu katika siku zilizopita hukuweza kutafuta kulingana na lengo Langu. Ninachotaka si dhana wala fikira za binadamu, sembuse pesa zako wala mali yako. Ninachotaka ni moyo wako, unaelewa? Haya ni mapenzi Yangu, na hata zaidi ni kitu ambacho Nataka kupata. 

Ijumaa, 12 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 56


Mwenyezi Mungu anasema, “Nimeanza kuchukua hatua kuadhibu wale ambao hufanya uovu, wale ambao hushika madaraka, na wale ambao hutesa wana wa Mungu. Kuanzia sasa kuendelea, yeyote anayenipinga katika moyo wake, mkono wa amri Zangu za utawala utakuwa daima juu yake. Fahamu hili! 

Ijumaa, 5 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 48


Mwenyezi Mungu anasema, “Mimi nina wasiwasi, lakini wangapi kati yenu wanaweza kuwa na nia moja na mawazo sawa na Mimi? Ninyi hamyasikilizi tu maneno Yangu, mkipuuza kabisa na kushindwa kuyatilia maanani, badala yake mkizingatia tu mambo yenu wenyewe ya juu juu. Mnachukulia kujali Kwangu kwa bidii na juhudi kama jitihada za bure; je, dhamiri yenu haiwahukumu? Ninyi ni wajinga na hamna mantiki; ninyi ni wapumbavu, na hamwezi kuniridhisha kabisa. 

Alhamisi, 4 Aprili 2019

"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (5) - Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia?




"Fichua Siri Kuhusu Biblia" (5) - Ni Vipi Kuna Makosa Ndani ya Biblia?


Watu wengi wanaamini kwamba Biblia yote imetiwa msukumo na Mungu, kwamba imetoka kabisa kwa Roho Mtakatifu, na kwamba hakuna hata neno moja lililo na kosa. Je, mtazamo wa aina hii unawiana na ukweli? Biblia iliandikwa na waandishi zaidi ya 40, yaliyomo yaliandikwa na kupangwa na mwanadamu, na haikufunuliwa moja kwa moja na Roho Mtakatifu. Ilikuwa vigumu kuepuka kuingiza mawazo na makosa ya mwanadamu wakati ambapo ilikuwa ikiandikwa na kupangwa na mwanadamu.

 Tazama Video: "Fichua Siri Kuhusu Biblia" (4) - Je, Biblia Nzima Imetiwa Msukumo na Mungu Kweli?

Jumamosi, 23 Machi 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa Makanisa | Sura ya 40

Maneno ya Roho Mtakatifu kwa Makanisa | Sura ya 40

Kwa nini ninyi ni wa mwendo wa polepole? Kwa nini hamsikii? Makumbusho kadhaa hayajawazindua; hili linanihuzunisha. Kwa kweli Sipendi kuwaona wanangu namna hii. Moyo Wangu unawezaje kustahimili hili? Ah! Lazima Niwafundishe kwa mkono Wangu mwenyewe. Mwendo Wangu unaendelea kuwa wa kasi. Wanangu! Inukeni haraka na mshirikiane na Mimi. Nani wanajitumia kwa dhati kwa ajili Yangu sasa? Ni nani anayeweza kujitolea kikamilifu bila malalamiko hata kidogo? 

Alhamisi, 14 Machi 2019

Matamshi ya Mungu | Sura ya 117

Matamshi ya Mungu | Sura ya 117

Mwenyezi Mungu anasema,“Wewe Ndiwe ambaye hufungua kitabu, Wewe Ndiwe ambaye hufungua mihuri saba, kwa sababu siri zote hutoka Kwako na baraka zote hufichuliwa na Wewe. Mimi sina budi kukupenda Wewe milele, na Mimi sina budi kuwafanya watu wote wakuabudu Wewe, kwa sababu Wewe ni nafsi Yangu, Wewe ni sehemu ya onyesho Langu kamili lenye ukarimu, sehemu ya msingi ya mwili wangu. Kwa hiyo, ni lazima Mimi Nitoe ushahidi maalum. Ni nani mwingine kando na yaliyo ndani ya nafsi Yangu anayefuata Moyo Wangu? 

Jumamosi, 26 Januari 2019

Matamshi ya Kristo | Sura ya 16

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Matamshi ya Kristo | Sura ya 16


Baada ya ushuhudiaji wa Mwana wa Adamu, Mwenyezi Mungu alijifichua kwetu hadharani kama Jua la haki. Haya ndiyo mabadiliko mlimani! Sasa inakuwa halisi zaidi na zaidi, na zaidi kuwa jambo la uhalisi. Tumeona utaratibu wa kazi ya Roho Mtakatifu, Mungu Mwenyewe ameibuka kutoka kwa mwili wa damu. 

Jumatatu, 21 Januari 2019

Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima | Sura ya 9

Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima | Sura ya 9


Mwenyezi Mungu anasema, "Kwa sababu kwamba wewe ni mmoja wa watu nyumbani Mwangu, na kwa sababu wewe ni mwaminifu katika Ufalme wangu, kila unachofanya lazima kifikie viwango Ninavyohitaji Mimi. Sisemi kwamba uwe tu kama wingu linalofuata upepo, bali uwe kama theluji inayong’aa, na uwe na hali kama yake na hata zaidi uwe na thamani yake. Kwa sababu Nilitoka katika nchi takatifu, si kama yungiyungi, ambalo lina jina tu na halina dutu kwa sababu lilikuja kutoka katika matope na si kutoka nchi takatifu. 

Jumatatu, 14 Januari 2019

Kazi na Kuingia (4)

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki,Mwenyezi Mungu

Kazi na Kuingia (4)

Ikiwa mwanadamu anaweza kuingia kabisa kulingana na kazi ya Roho Mtakatifu, maisha yake yatachipuka haraka kama mmea wa mwanzi baada ya mvua ya majira ya kuchipua. Kwa kuangalia kimo cha sasa wa watu wengi, hakuna mtu hata mmoja anayetilia mkazo umuhimu wa uzima. Badala yake, watu wanaweka umuhimu katika baadhi ya mambo ya juujuu yasiyokuwa na umuhimu. Au wanakimbia huku na kule na kufanya kazi bila malengo na ovyoovyo bila mwelekeo, hawajui waende njia gani na zaidi kwa ajili ya nani. "Wanajificha wenyewe katika unyenyekevu."

Jumapili, 13 Januari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (2)

 Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (2)

Kazi na kuingia kwenu ni duni kabisa; mwanadamu hafikirii kwamba kazi ni muhimu na hata yeye ni mzembe zaidi na kuingia. Mwanadamu haoni haya kuwa mafunzo mazuri anayopaswa kuingia ndani; kwa hivyo, katika uzoefu wake wa kiroho, kwa kweli yote ambayo mwanadamu huona ni njozi za kiajabu. Si mengi yanatakiwa kutoka kwenu kuhusu uzoefu wenu katika kazi, lakini, kama yule anayetakiwa kukamilishwa na Mungu, mnapaswa kujifunza kumfanyia Mungu kazi ili hivi punde muweze kuupendeza moyo wa Mungu.

Ijumaa, 11 Januari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (1)

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (1)


Tangu watu waanze kuikanyaga njia sahihi ya maisha, kumekuwa na mambo mengi ambayo bado hayajaeleweka vizuri. Bado wapo kwenye mkanganyiko kabisa kuhusu kazi ya Mungu, na kuhusu kiasi gani cha kazi wanapaswa kufanya. Hii, kwa upande mmoja, ni kwa sababu ya kuwa na uelekeo tofauti wa uzoefu wao na mipaka katika uwezo wao wa kupokea; kwa upande mwingine, ni kwa sababu kazi ya Mungu bado haijawaleta watu katika hatua hii. 

Ijumaa, 4 Januari 2019

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Utendaji (5)

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Utendaji (5)

Wakati wa Enzi ya Neema, Yesu alizungumza maneno kiasi na Akatekeleza hatua moja ya kazi. Kulikuwa na muktadha kwayo, na yalikuwa ya kufaa kwa hali za watu kwa wakati huo; Yesu alinena na kufanya kazi kama ilivyostahili muktadha wa wakati huo. Pia Alinena unabii kiasi. Alitabiri kwamba Roho wa ukweli angekuja wakati wa siku za mwisho, wakati ambapo Roho wa ukweli angetekeleza hatua ya kazi.